Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki

Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi Kanda ya Mashariki yalianza mwaka 1993 chini ya kilichokuwa Chama cha Wakulima Tanzania yaani “Tanzania Agricultural Society Organization” kwa kifupi TASO. Hata hivyo, kutokana na sababu za kiutendaji na kimaadili za TASO, kuanzia Mwaka 2017, Serikali ilitoa Mamlaka ya Usimamizi wa Uwanja kwa Sekretarieti za Mikoa ya Kanda ya Mashariki inayojumuisha Mikoa minne (4) ya Dar es Salaam, Morogoro, Pwani na Tanga.