Dira, Dhamira na Misingi Mikuu


Dira:

Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki kuwa kitovu cha ujuzi/teknolojia ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Ujasiriamali nchini

Dhamira:

Kuwawezesha wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali kufikia adhma yao kwa  kuimarisha ushirikiano katika uandaaji, utekelezaji na usimamizi wa mipango ya maendeleo ya uwanja; kuimarisha miundombinu ya kutolea huduma; kuruhusu mawazo mbadala na ubunifu; kuongeza na kudhibiti vyanzo vya mapato; kuimarisha ulinzi na usalama na kuboresha utoaji huduma

Maadili/Misingi Mikuu:

Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki yanazingatia msingi mikuu minane (6) ambayo ni:

  1. Ushirikishwaji wa wadau
  2. Ubunifu na Uthubutu
  3. Utendaji kazi uliotukuka
  4. Uwajibikaji wa pamoja na uwazi
  5. Haki na Usawa na; 
  6. Mwiko wa kutoa wala kupokea rushwa